Baadhi ya viongozi wa Jikomboe Youth Group wakifanya mazoezi na timu yao ya Netball Uwanja wa Nsumba.Hii ni moja ya njia ya kuwaunga mkono wachezaji wa timu hii changa ya netball ambao kwa kiasi kikubwa inaundwa na wachezaji wasichana ambao wengi wao hawakufanikiwa kuendelea na masomo.Wangeweza kukaa tu mtaani na kujiingiza kwenye maisha mabaya kama vile kujiuza,wizi matumizi ya madawa ya kulevya nk.Lakini kwa pamoja wame amua kuungana ili waweze KUJIKOMBOA kutokana na changamoto za maisha ya mtaani.Kupitia Jikomboe Youth Group wamekutanishwa pamoja na kwa umoja huu lazima WAJIKOMBOE.

0 comments:
Post a Comment