SHUGHULI ZETU


Jikomboe Youth Group ni kikundi cha vijana kilicho jikita katika shughuli zifuatazo ;

  • Kutoa mafunzo ya ujasiliamali namna ya kutambua na kutumia fursa mbalimbali zilizopo ili kuwezesha vijana kujiajiri wenyewe.
  • Tunahamasisha michezo mbalimbali ili kukuza vipaji na kuongeza ajira kupitia michezo mbalimbali.
  • Tunakemea na kutoa elimu kwa jamii juu ya matatizo mbalimbali yanayo ikabili jamii kama vile; Uharibifu wa Mazingira,Maambukizi ya virusi vya ukimwi unyanyasaji wa kijinsia,matumizi ya madawa ya kulevya nk.
  • Tunabuni na kuanzisha miradi mbalimbali ya kikundi ili kuwezesha kikundi kufanya shughuli zake na kutoa ajira miongoni mwa wanakikundi na jamii kwa ujumla.

0 comments:

Post a Comment